Habari

6/recent/ticker-posts

Header Ads Widget

Advertise with us here

NJIA INAYOTUMIKA KATIKA UPIMAJI WA BIKRA

                                         

Kipimo cha ubikra ni kipi?
hichi ni kipimo kinachotumika kupima kama mwanamke bado hajawahi kushiriki ngono na mwanaume yeyote tangu azaliwe.
vipimo hivi hufanyika mara kwa mara kwenye jamii za watu fulani fulani ambazo bikra huaminika kama ndio kipimo cha usafi na tabia nzuri kabla ya ndoa, nchini south africa vipimo hivi hufanyika kabla ya kupeleka wasichana kwenda kusoma nje ya nchi lakini pia kujaribu kuzuia maambukizi ya ukimwi ambayo yako juu sana nchini humo.
nchini misri mahakama kuu ya nchi hiyo iliamuru jeshi kuwapima wasichana wote bikra kabla hawajajiunga na jeshi la nchi hiyo.
lakini vipimo hivi vimepingwa sana na watetezi wa haki za binadamu wakidai kwamba vinashusha na kuaibisha utu wa mwanamke, baadhi ya watu kama wahindi na waarabu wamejikuta wakishiriki ngono kinyume na maumbile ili kuzuia bikra isitoke kabla ya ndoa.
mara nyingi bikra hii hupimwa kwanzia miaka sita mpaka umri wa kuweza kufunga ndoa katika jamii hizo, lakini pia hapa kwetu bado jamii inawaona mabikra ni watu wenye tabia nzuri kuliko hawa wengine.

bikra inapimwa vipi?
kipimo kinachoitwa kitaalamu kama two fingers virginity test ndio kinachotumika kuwapima wanawake hawa ubikra, mara nyingi madaktari hutumika kufanya vipimo hivi.
vidole viwili huingizwa ndani ya uke kuangalia ile ngozi laini kwa jina la hymen ambayo inaaminika kutoka na kuchanika mwanamke anaposhiriki ngono kwa mara ya kwanza, wakikuta ile ngozi haipo basi mwanamke huyo sio bikra na wakikuta ngozi ile ipo basi mwanamke huyo ni bikra.
mpaka sasa hivi hakuna mashine maalumu au kifaa maalumu kinachoweza kusema kwa uhakika kwamba mtu huyu ni bikra.
lakini pia baadhi ya makabila huweka shuka nyeupe kwenye kitanda siku ya ndoa, damu ikimwagika basi huamini mtu huyo alikua bikra.
sio rahisi kupima kama mwanaume ni bikra kwani wote wako sawa kimaumbile yaani mabikra na ambao sio mabikra.

changamoto za kipimo hichi ni zipi?
ngozi laini inayopimwa kutambua ubikra inaweza kuondolewa na baiskeli, kuendesha farasi au kufanya mazoezi mazito ya kukimbia na kuruka kamba, sasa mtu huyo anaweza kupoteza ngozi ile lakini kitaalamu yeye bado ni bikra kwani hajawahi kulala na mwanaume.
wasichana wengine huzaliwa na ile ngozi ikiwa ndogo sana kiasi kwamba hata siku ya ngono kwa mara ya kwanza damu zinaweza zisitoke kabisa lakini mwanamke huyu bado ni bikra.
baadhi ya wanawake ile ngozi inaweza kua ngumu sana na ikashindwa kutoka wakati wa ngono, kumbuka ngozi ile haizibiki kabisa tundu ndio maana damu za kila mwezi zinatoka hata kama mwanamke ni bikra.

je bikra inaweza kurudi baada ya kutoka?
ndio njia pekee ya kurudisha bikra ni kufanya upasuaji wa kuishona tena ile ngozi ya ndani ambayo inatambulika kama kipimo cha bikra, ngozi ile hushwona na baada ya mwezi mmoja hupona na mwanamke hua kama bikra tena. njia hizi wamekua wakitumia wanawake wanaotaka kuolewa haraka.                                          

je bikra inaweza kutoka bila maumivu?
kama wewe ni bikra na unashindwa kutoa bikra yako sababu ya maumvu makali basi kuna mabo ya kufanya kuzuia maumivu hayo, kwanza nunua mafuta maalumu kwa jina la k gel ambazo hulainisha zaidi uke kuruhusu uume kupita, pia kuna dawa za nganzi za kupaka kwa jina la lidocaine cream ambazo zikipakwa saa moja ndani ya uke kabla ya tendo hupunguza maumivu kwa kiasi kikubwa sana.                          

Kwa maelezo zaidi na habari nyengine za kiafya tembelea tovuti ya SIRI ZA AFYA BORA

Post a Comment

7 Comments

  1. Jee vidole viwili vikiingia ukeni ndio maana ake hauna bikra?

    ReplyDelete
    Replies
    1. Kiukweli kama ni bikra, vidole viwili haviwezi ingia ukeni kirahisi.

      Delete
    2. Sasa hizo k gel znapatikanaz wap

      Delete
  2. Kadr unavyokaa na bikra ndvyo inazd kuwa ngumu kutoka??

    ReplyDelete
  3. namm naomba kuuliza hv dalili 1 yakua na bikra ni kuingiza vidole vidole viwili visiingie? ndo unakua upo bikra mn nimewahi ckia kwamba kidole 1 kinaweza ingia ila viwili hpn

    ReplyDelete
  4. Sas hizo k gel na lidocaine cream zinapatikana maduka gn

    ReplyDelete
    Replies
    1. Matatizo ya tumbo la uzazi & ugumba & kutokwa na. Maji na uchafu ukeni $ kunuka uke & kubana uke mkubwa. Wasiliana na dr 0676039091

      Delete

Youtube Channel Image
Hajiizo Subscribe To watch more
Subscribe