Habari

6/recent/ticker-posts

Header Ads Widget

Advertise with us here

Radi yawaua watu wengi kanisani Rwanda

map showing Rwanda and Burundi with the former's capital Kigali marked out.

Radi imewaua takriban watu 16 na kuwajeruhiwa wengine kadhaa kwenye kanisa moja la KiAdiventista nchini Rwanda siku ya Jumamosi
Wengi wa waathiriwa walifariki papo hapo wakati radi ilipiga kwenye kanisa katika wilaya iliyo kusini mwa nchi ya Nyaruguru, kwa mujibu wa meya wa eneo hilo, Habitegeko Francois.
Watu wawili walifariki kutokana na majeraha, na watu 140 walikimbizwa hospitalini na vituo vya afya.
Radi pia ilimuua mwanafunzi eneo hilo siku ya Ijumaa kwa mujibu wa meya.
Ajali hiyo katika eneo lenye milima karibu na mpaka na Burundi, ilitokea saa za mchana wakati waumini walikuwa bado ndani ya kanisa.
Madaktari wanasema kuwa watu wangine watatu wako hali mahututi lakini wanapata nafuu, Bw Francois aliiambia AFP.
Alisema kuwa katika kisa cha siku ya Ijumaa, radi ilipiga kundi la wanafunzi 18 eneo hilo na kumuua mmoja.
Watatu kati ya wanafunzi hao wamebaki hospitalini huku wengine wakiruhisiwa kwenda nyumbani.
SOURCE: BBC SWAHILI

Post a Comment

0 Comments

Youtube Channel Image
Hajiizo Subscribe To watch more
Subscribe