Habari

6/recent/ticker-posts

Header Ads Widget

Advertise with us here

MAKALA: Serikali ya India Yazuia Mitandao ya Ngono Kupatikana Nchini Humo

Katika hali ya ghafla Serikali ya India imetoa agizo la kuzuia mitandao inayoeneza picha, video n.k za ngono kupatikana nchini India. Mara moja watoa huduma wa intaneti mbalimbali wameanza kufuata agizo hilo. Uamuzi huo ambao ukaanza kulaaniwa na wengi mara moja umekuja baada ya maombi ya watu kadhaa kuwepo mahakani tayari kwa muda mrefu ya kupinga upatikanaji wa mitandao ya mambo ya ngono nchini India.



Kupitia mitandao ya kijamii tayari watu wengi nchini humo wameungana katika kupinga uamuzi huo wa serikali ya India kuzuia (ban) zaidi ya mitandao 850 ya kingono ikiwepo maarufu zaidi kama vile PornHub, YouPorn na mingine mingi.
Wengi wanasema uamuzi huo unaingilia uamuzi wa mtu binafsi huku wakidai hawaoni jinsi mtu anavyovunja sheria au kufanya makosa pale anapokuwa chumbani/nyumbani kwake na kuangalia picha hizo. Wanadai uamuzi huo wa serikali unaingilia haki ya uhuru binafsi wa wananchi ambao unalindwa kikatiba.

Tayari baadhi ya watoa huduma za internet washaanza kufuata agizo la serikali lakini bado wengine wamekataa wakisema watakuwa wanavunja haki za wateja wao. Watafiti mbalimbali wanasema uamuzi wa serikali ata ukifuatwa hautaweza kuwa na nguvu sana kwani watu wanaweza jifunza kutumia teknolojia za maficho kama vile ya VPN ambazo zitawawezesha kutembelea mitandao hiyo bila tatizo huku watoa huduma za intaneti na serikali kutokuwafahamu kabisa.

Wanaounga mkono maamuzi hayo wanadai uwepo wa mitandao hiyo unachangia katika uwepo na ukuaji wa makosa ya kingono kama vile ubakaji.

Je, kwa mtazamo wako unadhani sheria kama hii ingeletwa Tanzania ingepunguza ongezeko la vitendo vya ubakaji na uasharati?
 

Post a Comment

0 Comments

Youtube Channel Image
Hajiizo Subscribe To watch more
Subscribe