Habari

6/recent/ticker-posts

Header Ads Widget

Advertise with us here

Facebook Wanakupa Uhuru wa Kuchagua Marafiki Wakuu

Facebook imeamua kumruhusu kila mtu aamue ni habari za aina ipi anataka kuziona kwenye kurasa yake. Hii inawezekana kwa kipengengele kipya walichokiongeza, kinachokuruhusu kuchagua marafiki wako unaopenda kuona habari zao awali ya habari zote zingine kwenye kurasa yako punde unapoingia kwenye mtandao huo wa kijamii.

kuu ya badiliko hili jipya kutoka Facebook ni kwamba huna haja ya kushuka chini sana kwenye skrini ama kurasa yako kuona habari unazopenda zaidi. Hili ni jambo la kitofauti sana kutoka kwa Facebook, kampuni iliyozoeleka kuwa na usiri wa hali ya juu kuhusu namna wanavyochagua kukupa habari za marafiki na kampuni upendazo na wanafanya hivi kupitia kitu kinachojulikana kama ‘The Facebook Algorithm’ . Ili kutumia mabadiliko ya Facebook yaliyoelezwa hapa, ingia kwenye News ‘Feed Preferences’, chaguzo iliyo ndani ya menu karibu na eneo la taarifa pale juu, kulia kwenye kurasa au app yako ya facebook.

Utaona orodha ya watu ama kurasa uloziziona karibuni au zile unazozitembelea mara nyingi.
Ukifanikiwa kuchagua mipangilio ya kukufaa, utaweza kuona habari za hao marafiki na kurasa uzipendazo kwanza kabla ya habari za watu wengine. Kwa kweli, kwa hili la kitofauti la kutoka kwa facebook, unaweza kuona kidogo faida au labda tuseme raha, ya Facebook kwani utapata muda wote kile unachotaka.

Kwa ujumla hii ni habari nzuri, na pengine cha kufurahisha zaidi ni kwamba chaguo lako la watu unaotaka kuona ni siri yako, halitojulikana kwa wengine. Hakuta kuwa na wasiwasi kwamba mtu mwingine atajua kwamba hauwekei maanani ‘update’ zinazotoka kwake.

Post a Comment

2 Comments

Youtube Channel Image
Hajiizo Subscribe To watch more
Subscribe