Habari

6/recent/ticker-posts

Header Ads Widget

Advertise with us here

Makala: Mambo 10 ya kujiepusha nayo ili Sheria ya Mitandao isikufunge

Sheria ya mitandao inaanza kutumika rasmi
tarehe 1 septemba 2015, haya mambo 10
muhimu ili sheria hii isikukamate
1. Epuka Kusambaza ujumbe wa uchochezi ama ushawishi wa kisiasa unaoweza kuleta athari kwa jamii yetu kupitia mitandao
2. Epuka Kusambaza au kutunga ujumbe unaoleta uchochezi wa kidini unaoweza kupelekea kuvuruga amani na maelewano kwa jamii kupitia mitandao
3. Epuka Kusambaza picha ama video za utupu ama zilizokosa maadili kwa jamii kupitia mitandao mbalimbali (Whatsapp,Facebook,Youtube,Instagram n.k
4. Epuka Kusambaza picha ama video za uchochezi wa kidini ama kisiasa kupitia makundi
mbalimbali ama mitandao ya kijamii
5. Epuka Kushiriki kusambaza chochote kati ya vilivyotajwa hapo juu ( kutuma kama ulivyopokea ) itakugharimu
6. Epuka Wizi kupitia mitandao mbalimbali na mitandao ya simu utakugharimu
7. Epuka Kumpatia mtu line yako ya simu na kutumika kufanyia wizi ama utapeli itakugharimu
8. Epuka Kushiriki kumchafua MTU,taasisi,kikundi cha watu kwa namna yoyote kupitia mitandao pia
itakugharimu
9. Epuka Kupoteza simu bila kutoa taarifa na kufunga mawasiliano hayo yanaweza kupelekea kutumika kufanya uhalifu na ukaangukia hatarini
10. Epuka Kutumia mtandao kwa utapeli kupitia 'brand' ama jina la mtu itakugharimu

Hukumu: Ni kifungo cha miaka kadhaa gerezani
ama faini ya fedha isiyopungua milioni 5
kulingana na kosa lililofanyika

Post a Comment

0 Comments

Youtube Channel Image
Hajiizo Subscribe To watch more
Subscribe