Habari

6/recent/ticker-posts

Header Ads Widget

Advertise with us here

FAHAMU Mtoto 1 kati ya watoto 2 wanaozaliwa ni wanaharamu

 
 bbcswahili.com

Je ndoa imepoteza hadhi yake?

Watoto waliozaliwa nje ya ndoa walikuwa wanatambulika kama wana haramu.
Lakini takwimu za hivi punde zinaonesha kuwa mtazamo huo umebadilika kadri walimwengu wanavyoendelea kukubali maisha ya kisasa.

Takwimu za hivi punde nchini Uingereza zinaonyesha kuwa mmoja kati ya watoto wawili wanaozaliwa Uskochi Kaskazini mwa Uingereza ni vizazi vya kina mama ambao hawajaolewa na baba za watoto wao.

Hii ni kumaanisha kuwa asilimia 50% ya wanawake wanaojifungua hawajafunga ndoa.
Katika maeneo ya Kaskazini mwa Uingereza asilimia 60 ya wanawake wanaojifungua watoto wao hawajafunga ndoa.

Aidha asilimia 60% ya watu wanawekana kinyumba;hawana vyeti vya ndoa.
Kwengine katika muungano wa mataifa ya Uingereza asilimia 50 ya watu wanasusia kufunga ndoa kihalali.
Katika miaka ya 1940, asilimia 94 ya watoto wote walikuwa wanazaliwa ndani ya ndoa.

Kwa mujibu wa idara ya utafiti wa taifa, idadi hiyo ya juu inaelekea kutoshana na ile ya mataifa ya bara Uropa kama vile Ufaransa ambapo asilimia kubwa ya watoto wanaozaliwa huko hawako katika familia za kudumu.
Takwimu hii inasadifiana na ile ya mataifa kusini mwa Marekani ambapo watafiti wamekuwa wakilaumu kuongezeka maradufu kwa mimba za mapema hususan katika maeneo yenye idadi kubwa ya umasikini katika jamii na uhaba wa ajira na kitega uchumi.
Kimsingi,wataalamu wa maswala ya jamii katika mataifa ya Marekani ya Kati wamekuwa wakitafiti uhusiano kati ya idadi kubwa ya mimba na watoto wanaozaliwa nje ya ndoa na umasikini.
Aidha kuna uhusiano mkubwa kati ya idadi kubwa ya mimba za mapema na watoto wanaozaliwa nje ya ndoa.
Utafiti huo umebaini kuwa asilimia, 72% ya watoto wanaozaliwa miongoni mwa wamarekani weusi ni wanaharamu.

Miongoni mwa wamarekani weupe idadi hiyo ni asilimia 29% pekee.
Hata hivyo Idadi ya watoto wanaozaliwa nje ya ndoa miongoni mwa wamarekani waliochanganya asili ni 66%.

Asili mia 17% ya watoto wanaozaliwa miongoni mwa jamii ya Wahindi wanazaliwa nje ya ndoa.
Takwimu hii ni kwa mujibu wa utafiti wa mwaka huu 2015 Child Trends Databank.

Kutokana na hali ngumu ya maisha na idadi kubwa ya vijana ambao hawana kazi mahitaji ya ndoa yamezidi makadirio yao ya kifedha hivyo wanaona afadhali kuishi kinyumba tu pasi na ndoa rasmi.

HABARI KAMILI IKO HAPA >>>> BBC

Post a Comment

0 Comments

Youtube Channel Image
Hajiizo Subscribe To watch more
Subscribe